Website ni mkusanyiko wa kurasa za wavuti (web pages) zinazoonekana kupitia mtandao kwa kutumia kifaa kama simu au kompyuta. Kurasa hizi huwa na taarifa, picha, video, fomu au huduma mbalimbali kwa watumiaji. Website inaweza kuwa ya mtu binafsi, kampuni, taasisi ya elimu au hata serikali.

Mifano ya website:

Google – injini ya utafutaji maarufu duniani.

YouTube – tovuti ya kushiriki video.

Wikipedia – ensaiklopidia ya mtandaoni.

TCRA – tovuti ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania.

Facebook – mitandao ya kijamii.

Website ni njia muhimu ya kuwasiliana, kufundisha, kuuza bidhaa au kutoa huduma mtandaoni.